Tuesday, November 20, 2012

BECKHAM KUIKACHA GALAXY MWISHONI MWA MSIMU.

Nahodha wa zamani wa Uingereza, DAVID BECKHAM anatarajiwa kuondoka katika klabu ya Los Angeles Galaxy mwezi ujao baada miaka sita kucheza katika Ligi Kuu nchini Marekani maarufu kama Major League. Nyota huyo amepanga kuikacha klabu hiyo baada ya msimu wa ligi hiyo kumalizika Desemba 1 mwaka huu. Katika taarifa yake BECKHAM mwenye umri wa miaka 37 amesema kuwa anahitaji changamoto nyingine kabla ya kuamua rasmi kustaafu soka. Klabu ya Melbourne Heart ya Australia imedai kuwa ipo katika mazungumzo na nyota huyo ili wamsajili kwa ajili ya mechi 10 nyota huyo pamoja na mwenyewe kudai kuwa hana mpango wa kucheza soka katika Ligi Kuu ya nchini humo maarufu kama A League. BECKHAM alianza kucheza soka katika klabu ya Manchester United ambapo akiwa hapo alifanikiwa kushinda taji la Ligi Kuu nchini Uingereza mara sita pamoja na taji moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya kutua Real Madrid mwaka 2003 na baadae Marekani mwaka 2007.

No comments:

Post a Comment