Saturday, November 24, 2012

MENEZES ATIMULIWA KUINOA BRAZIL.

Shirikisho la Soka nchini Brazil limetangaza kusitisha mkataba na kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo Mano Menezes. Menezes amekuwa akiandamwa na wadau wengi wa soka nchini Brazil kwa kushindwa kuifanya timu kurejesha makali yake ya miaka ya nyuma kitu mara nyingi shirikisho la nchi hiyo limekuwa likifumbia macho lawama hizo. Kocha huyo ambaye amechukua mikoba ya kuinoa timu hiyo mwaka 2010 amekuwa akiandamwa kwa kushindwa kuiongoza Brazil kunyakuwa medali yake ya kwanza ya dhahabu katika michuano ya olimpiki iliyofanyika jijini London mwaka huu pamoja na kutolewa kwa timu hiyo kushiriki michuano ya Copa America mwaka 2011. Shirikisho hilo limesema kuwa kocha mpya ambaye atachukua nafasi ya Menezes atatangazwa mapema Januari mwakani.

No comments:

Post a Comment