Saturday, November 24, 2012

ARSENAL YALAMBA MKATABA MNONO.

KLABU ya soka ya Arsenal, imekubali kuongeza mkataba wenye thamani ya paundi milioni 150 kwa ajili ya udhamini wa fulana wa kampuni ya ndege ya Emirates. Mkataba huo mpya ambao utamalizika mwishoni mwa msimu wa 2018-2019 utakuwa na thamani ya paundi milioni 30 mwaka kwa timu hiyo inayotoka kaskazini mwa jiji la London. Ofisa Mkuu wa klabu hiyo Ivan Gazidis alithibisha katika wavuti wao juu makubaliano yaliyofikiwa katika mkataba huo mpya ambao utaifanya kuwa mojawapo ya vilabu zenye mikataba minono ya fulana zake. Gazidis ameapa kuwa meneja wa klabu hiyo Arsenal Wenger atapewa sehemu ya pesa hizo ili kuimarisha kikosi chake kiweze kukata kiu ya mashabiki wake kwa kunyakuwa kombe mwishoni mwa msimu. Chini ya mkataba huo kampuni ya Emirates itaendelea kutumia jina lake katika uwanja wa Arsenal mpaka 2028.

No comments:

Post a Comment