Saturday, November 24, 2012

REDKNAPP KUINOA QPR.

HARRY Redknapp ametajwa kuwa meneja mpya wa klabu ya Queens Park Rangers kufuatia kutimuliwa kwa aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Mark Hughes. Redknapp ambaye alitimuliwa katika klabu ya Tottenham Hotspurs June mwaka huu amesaini mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo ambayo haijashinda mchezo hata mmoja katika Ligi Kuu nchini Uingereza msimu huu. Katika taarifa iliyotumwa katika wavuti wa klabu hiyo wasaidizi wa Hughes, Mark Bowen na eddie Niedzwiecki ndio watakaokuwa makocha wa muda wakati wa mchezo dhidi ya Manchester United na Redknapp atakuwa akitazama mchezo huo jukwaani. Akihojiwa mara baada ya uteuzi huo Redknapp mwenye umri wa miaka 65 amesema kuwa amefurahishwa kuinoa klabu hiyo pamoja na changamoto zilizopo mbele yake za kuhakikisha klabu hiyo inarejesha makali yake ili kuepuka balaa la kushuka daraja.

No comments:

Post a Comment