Saturday, November 24, 2012

ABOU-TRIKA AMONG THREE NOMINEES OF AFRICAN BASED PLAYER OFO THE YEAR AWARD.

SHIRIKISHO la Soka barani Afrika-CAF limetangaza orodha ya majina matatu ya wachezaji wanaocheza soka barani Afrika watakaogombania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2012. Majina hayo yaliyotajwa na CAF ni pamoja na wachezaji wa kimataifa wa Zambia ambao wanacheza katika klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Reinford Kalaba na Stopila Sunzu pamoja na nyota wa kimataifa wa Misri na klabu ya Al Ahly Mohamed Abou-Trika. Wachezaji nyota wa timu ya Esperance ya Tunisia Youssef Msakni na Tannick N’Djeng waliachwa katika orodha hiyo pamoja na kukiongoza kikosi cha timu hiyo katika mchezo wa fainali wa Ligi ya Mabingwa ya Afrika ambao walipoteza kwa Al Ahly kwa mabao 3-2. Mshindi wa tuzo hiyo atatangazwa katika sherehe zitakazofanyika jijini Accra, Ghana Desemba 20 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment