Sunday, November 25, 2012

MOURINHO ALIA NA MWAMUZI.

BAO lililofugwa na Benat Etxebarria jana usiku liliipa ushindi wa kushangaza wa bao 1-0 dhidi ya Real Madrid katika mchezo uliochezwa jijini Seville na kuwaacha mabingwa hao watetezi nyuma kwa alama nane kwa Barcelona ambao wanaongoza La Liga huku wakiwa bado na mchezo mmoja mkononi. Matokeo hayo yanaifanya Madrid kubakia katika nafasi ya tatu wakiwa wamejikusanyia alama 26, huku wakiwa wamepitwa alama tano na Atletico Madrid ambao wanashika nafasi ya pili. Mahasimu wa Madrid, Barcelona wanaweza kuongeza pengo na kufikisha alama 11 kama wakiwafanikiwa kushinda mchezo wao wa baadae leo dhidi ya Levante ambao wanashika nafasi ya sita. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo meneja wa Madrid Jose Mourinho amelaumu waamuzi kwa kushindwa kumudu mchezo huo na kuonyesha upendeleo kwa wapinzani wao kitu ambacho kilichangia kwa kiasi wao kupoteza mchezo huo muhimu.

No comments:

Post a Comment