Sunday, November 25, 2012

BOLT, FELIX WANYAKUWA TUZO YA WANARIADHA BORA WA MWAKA.

WANARIADHA nyota wanaoshikilia medali za dhahabu katika michuano ya Olimpiki, Usain Bolt na Allyson Felix wamenyakuwa tuzo ya wanariadha bora wa mwaka kwa wanaume na wanawake. Wanaridha hao walitunukiwa tuzo hizo na Shirikisho la Riadha la Kimataifa-IAAF katika sherehe zilizofanyika jijini Barcelna, Hispania jana. Bolt ambaye ni raia wa Jamaica alifanikiwa kutetea medali zake katika mbio za mita 100 na 200 jijini London anakuwa mwanaridha wa kwanza kushinda tuzo hiyo mara nne mfululizo. Katika michuano ya olimpiki Felix alinyakuwa medali tatu za dhahabu na kufanikiwa kunyakuwa tuzo hiyo mbele ya Jessica Ennis wa Uingereza ambaye naye alikuwepo katika orodha ya mwisho ya wawanariadha wanaogomea tuzo hiyo. 
Felix ambaye anatoka Marekani alifanikiwa kunyakuwa medali za dhahabu katika mbio za mita 200 na pia alikuwa sehemu ya wanariadha walioshinda mbio za kupokezana vijiti za mita 100 na 400 hivyo kuwa mwanamke wa kwanza kushinda medali tatu za dhahabu katika michuano hiyo toka mwaka 1988.

No comments:

Post a Comment