Sunday, November 25, 2012

GUARDIOLA AIMEZEA MATE BRAZIL.

MENEJA wa zamani wa klabu ya Barcelona, Pep Guardiola atafurahi kama akipewa kibarua cha kuinoa Brazil ambayo wiki iliyopita ilimtimua kocha wake Mano Menezes. Tetesi hizo Guardiola kutaka kuinoa Brazil ziliandikwa na gazeti la michezo la Lance ambalo lilidai kutoa taarifa hizo kwa mtu wa karibu wa kocha huyo. Guardiola ambaye aliifundisha Barcelona kwa mafanikio baada ya kuchukua mikoba ya kuinoa kutoka kwa Frank Rijkaard mwaka 2008, aliamua kuacha kuifundisha timu hiyo katika kipindi cha majira ya kiangazi na kuamua kupumzika. Katika kipindi cha miaka minne ambayo amekuwa akiinoa Barcelona, Guardiola amefanikiwa kunyakuwa mataji 14 yakiwemo mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment