Sunday, November 25, 2012

SNEIJDER HATIHATI INTER.

MENEJA wa michezo wa klabu ya Inter Milan, Marco Branca amependekeza kuwa kiungo Wesley Sneijder hatachezeshwa mpaka atakapokubali kuongeza mkataba wake. Kiungo huyo wa kimataifa kutoka Uholanzi mwenye umri wa miaka 28 amekuwa nje ya uwanja toka Septemba mwaka huu baada ya kuumia amekuwa akihusishwa na taarifa za kuondoka katika klabu hiyo katika kipindi cha dirisha dogo la usajili Januari mwaka huu. Sneijder alihusishwa na taarifa za kuhamia Uingereza katika klabu ya Manchester United mwaka 2011 lakini alikanusha tetesi hizo na kudai hajafanya mazungumzo rasmi juu ya kuhamia huko. Branca amesema kuwa kwasasa watakuwa wavumilivu wakati wakiangalia uwezekano wa kumshawishi nyota huyo ili aongeze mkataba utakaomuwezesha kubakia klabuni hapa kwa muda zaidi. Sneijder alijiunga na Inter Milan mwaka 2009 akiwa amecheza katika vilabu vya Ajax Amsterdam ya Uholanzi na Real Madrid ya Hispania.

No comments:

Post a Comment