Sunday, November 25, 2012

HATTON ASTAAFU NGUMI KWA MARA YA PILI BAADA YA KIPIGO.

BONDIA Ricky Hatton kutoka Uingereza mbaye amewahi kuwa bingwa wa dunia wa uzito wa Light Weight ametangaza kustaafu tena mchezo huo baada ya kupewa kipigo na Vyacheslay Senchenko katika pambano lililofanyika jijini Manchester. Hatton mwenye umri wa miaka 34 hajapigana toka mwaka 2009 lakini kurejea kwake ulingoni baada ya muda huyo kuliishia katika raundi ya tisa katika pambano hilo lililofanyika Jumamosi. Bondia anadai kuwa alikuwa akihitaji pambano moja ili kuona kama anaweza kurejesha makali yake kama zamani lakini hilo limeshindikana hivyo hana budi kuachana na mchezo huo ili kufanya mambo mengine. Hatton alitangza kurejea ulingoni Septemba mwaka huu ikiwa ni miezi 14 toka alipotangaza kustaafu mchezo huo kwa mara kwanza. Pambano la mwisho kucheza kabla ya kuamua kuachana na mchezo huo lilikuwa dhidi ya Manny Pacquiao lililofanyika jijini Las Vegas, Marekani mwaka 2009 ambalo alipoteza. 

No comments:

Post a Comment