Monday, November 26, 2012

"FULECO" MWANASESERE WA KOMBE LA DUNIA 2014.

SHIRIKISHO LA Soka Duniani-FIFA limetoa jina la Fuleco kwa mwanasesere utakaotumika katika michuano ya Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil, neno ambalo waandaji wamesema kuwa linahusu ufahamu wa mazingira. Karibu nusu ya watu zaidi ya milioni 1.7 ambao walipiga kura katika mitandao walichagua jina Fuleco tofauti na mengine yaliyokuwepo katika kinyang’anyiro hicho ya Zuzeco na Amijubi. Utamaduni wa kuwa na mwanasesere katika Kombe la Dunia ulianza mwaka 1966 wakati wa michuano iliyofanyika Uingereza ambayo waliipa jina la World Cup Wille. Toka kipindi hicho wanasesere wamekuwa wakionekana katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1974 iliyofanyika Ujerumani ambao iliitwa Tip Tap ikimaanisha wavulana wawili wa nchi hiyo, Pique ikimaanisha pilipili katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Mexico mwaka 1986 na Zakumi ikimaanisha Chui jina ambalo lilitumika katika michuano ya Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini. Fuleco anatarajiwa kuonekana rasmi jijini Sao Paulo baadae wiki hii katika sherehe za upangaji wa ratiba ya michuano ya Kombe la Shirikisho ambayo itafanyika Juni mwakani.

No comments:

Post a Comment