Monday, November 26, 2012

MBIO ZA UBINGWA BADO HAZIJAISHA - VILANOVA.

MENEJA wa klabu ya Barcelona, Tito Vilanova amesisitiza kuwa mbio za ubingwa wa Ligi Kuu nchini Hispania maarufu kama La Liga bado hazijaisha pamoja na kikosi chake kuongeza pengo la alama 11 na mabingwa watetezi wa ligi hiyo Real Madrid. Barcelona ilifanikiwa kupata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Levante jana usiku na kutumia nafasi baada ya Real Madrid kupoteza mchezo wao wa Jumamosi kwa kufungwa na Real Betis kwa bao 1-0. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Vilanova aliwapongeza wachezaji kwa kuonyesha juhudi na kuihakiikishia ushindi timu lakini akasisitiza kuwa mbio za ubingwa bado kwakuwa wapo Atletico Madrid ambao wanafuatia katika nafasi ya pili kwa tofauti ya alama tatu pekee. Kocha huyo aliendelea kusema kuwa Atletico wameanza msimu vizuri kitu ambacho sio cha kushangaza kwasababu walimaliza msimu uliopita wakiwa katika kiwango cha juu hivyo inabidi kuhakikisha wanelekeza nguvu zao kushinda kila mchezo ili kuendelea kukalia usukani wa La Liga.

No comments:

Post a Comment