Monday, November 26, 2012

VETTEL AFANIKIWA KUTETEA TAJI LA DUNIA.

DEREVA nyota wa mbio za Langalanga wa timu ya Red Bull, Sebastian Vettel amefanikiwa kushinda taji la dunia la tatu mfululizo kwa tofauti ya alama tatu katika michuano ya Brazil Grand Prix. Katika tukio ambalo mbio hizo ziliathiriwa na mvua, Vettel alipambana na kufanikiwa kumaliza katika nafasi ya sita baada ya kuporomoka mpaka nafasi ya mwisho katika mzunguko wa kwanza kufuatia kupata ajali. Mpinzani wake katika mbio hizo Fernando Alonso wa Ferrari alimaliza katika nafasi ya pili ambapo alikuwa akihitaji Vettel kumaliza chini ya nafasi ya saba ili aweze kunyakuwa taji la dunia. Dereva wa timu ya Force India, Nico Hulkenberg alikatwa alama baada ya gari lake kupoteza mwelekeo na kumgonga Lewis Hamilton wakati akijaribu kumpita dereva huyo wa timu ya McLaren. Vettel anakuwa dereva mdogo zaidi katika historia kushinda mataji matatu ya dunia akizidiwa miaka sita na Ayrton Senna ambaye ndiye dereva watatu kushinda mataji matatu mfululizo.

No comments:

Post a Comment