Friday, November 23, 2012

NI BAHATI KWA BANITEZ KUPEWA CHELSEA WAKATI WA CLUB WORLD CUP - FERGUSON.

MENEJA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amesema kuwa ni bahati kwa Rafael Banitez kuteuliwa kukinoa kikosi cha Chelsea wakati ambapo wanakaribia kwenda kushiriki michuano ya Klabu Bingwa ya Dunia. Banitez ambaye amewahi kuifundisha Liverpool alichukua nafasi ya Roberto Di Matteo ambaye alitimuliwa Jumatano baada ya kuifundisha kwa kipindi cha miezi nane. Benitez alifanikiwa kunyakuwa taji la michuano hiyo muda mfupi baada ya kupewa mikoba ya kuinoa Inter Milan ya Italia na anaweza kufanya hivyo tena akiwa na Chelsea mwezi ujao. Ferguson amesema kuwa katika CV za Banitez anaweza kuwa na vikombe viwili vya Klabu Bingwa ya Dunia bila kufanya kazi kubwa ya kujenga timu akitolea mfano kocha huyo aliposhinda taji la michuano hiyo wakati alipochukua timu kutoka kwa Mourinho. Kombe la Klabu Bingwa ya Dunia ni michuano ambayo hushirikisha mabingwa wa vilabu kutoka mabara sita duniani.

No comments:

Post a Comment