Friday, November 23, 2012

SINA URAFIKI NA RONALDO NJE YA UWANJA - ALONSO.

KIUNGO nyota wa Real Madrid, Xabi Alonso amekiri kuwa hana urafiki wa karibu na mshambuliaji nyota wa hiyo Cristiano Ronaldo lakini wamekuwa wakiheshimiana kwakuwa wanafanya kazi pamoja. Toka mwanzoni mwa msimu kumekuwa na tetesi katika kambi ya Madrid baada ya mchezaji huyo kuonyesha hana furaha kuwepo klabuni hapo hadharani. Alonso ambaye ni kiungo wa zamani wa Liverpool amekuwa wa kwanza kuweka wazi mahusiano aliyonayo na nyota huyo wa zamani wa Manchester United na kukiri kuwa urafiki wao ni pindi wawapo uwanjani lakini baada ya hapo kila anashika hamsini zake. Pamoja na kukiri kutokuwa na urafiki wa karibu na Ronaldo lakini alimsifia nyota kuwa ni mchezaji wa kiwango cha juu na amekuwa msaada mkubwa katika kikosi hicho kinachonolewa na kocha Jose Mourinho. Alonso pia alimsifia Mourinho kwamba ni kocha bora na amejifunza mengi kutoka kwake tofauti na watu wengi wasiomfahamu wanavyomchukulia.

No comments:

Post a Comment