Thursday, November 15, 2012

PELE ARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI.

MWANASOKA nguli wa zamani wa Brazil, Pele amewashukuru mashabiki wake ambao walionyesha kuguswa na kuugua kwake baada ya kuruhusiwa kutoka Hospitali jana. Pele mwenye umri wa miaka 72 alifanyiwa upasuaji wa nyonga katika hospitali ya Albert Einstein iliyopo jijini Sao Paulo na kuruhusiwa nyumbani baada ya matibabu kumalika kwa mafanikio. Mara baada ya kuruhisiwa kutoka hospitali Pele alitumia muda huo kuwashukuru mashabiki wake kwa kuonyesha upendo mkubwa kwake toka alipolazwa. Nguli aliondoka hospitalini akiwa katika baiskeli ya magurudumu na atahitaji kutumia magongo kwa ajili ya kumsaidia kutembea wakati kidonda chake kikipona na pia ameshauriwa kupumzika kwa miezi kadhaa.

No comments:

Post a Comment