Friday, November 16, 2012

PUYOL FITI KUIKABILI ZARAGOZA.

NAHODHA wa klabu ya Barcelona, Carles Puyol anatarajiwa kurejea uwanjani ikiwa ni siku 45 zimepita toka alipoumia kiwiko cha mkono wake wa kulia. Puyol mwenye umri wa miaka 34 anarejea wakati ambapo timu hiyo iitakuwa wageni wa Real Zaragoza katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Hipania maarufu kama La Liga na uwepo unatarajia kuimarisha safu ya ulinzi ambayo imekuwa ikiyumba kwa kuwakosa nyota wake. Beki mwingine nyota wa timu hiyo Gerard Pique naye alirejea uwanjani wiki iliyopita baada ya kuwa nje kwa wiki saba akisumbuliwa na majeraha ya mguu. Msimu uliopita Barcelona iliruhusu nyavu zake kutikiswa mara 29 pekee katika michezo 38 ya La Liga waliyocheza na kumaliza katika nafasi ya pili mbele ya Real Madrid lakini msimu huu tayari wameshakubali kufungwa mabao 14 katika michezo 11 pekee waliyocheza.

No comments:

Post a Comment