Monday, November 26, 2012

TEVEZ AFUNGIWA KUENDESHA GARI.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Manchester City, Carlos Tevez amenyang’anywa leseni ya kuendeshea gari baada ya kushindwa kutoa vielelezo vilivyohitajika baada ya gari lake kukamatwa likiwa katika mwendo wa kasi. Gari la Tevez lilivuka kiwango cha mwendo kasi kilichowekwa katika mji wa Morecambe, kaskazini mwa jiji la London Machi 28 mwaka huu wakati wachezaji wa akiba wa City walipokwenda kucheza dhidi ya wachezaji wa akiba wa timu ya Morecambe. Wakili wa nyota huyo wa kimataifa wa Argentina, Gwyn Lewis aliwaambia mahakimu wa Lancaster kuwa mteja wake alikubali kuwa hakuwakilisha vielelezo vyovyote kuhusiana na tukio na kwa kosa hilo ndio mahakama ikapelekea kumpa adhabu hiyo. Tevez ambaye alipokea taarifa hizo asubuhi jana hakuwepo wakati wa usikilizaji wa shauri lake hilo na muda kamili ambao atafungiwa leseni yake utajulikana Desemba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment