Tuesday, November 27, 2012

GERRARD, LAMPARD MIONGONI KATIKA ORODHA YA VIUNGO 15 WA FIFPRO 2012.

VIUNGO nyota wa kimataifa wa Uingereza, Steven Gerrard na Frank Lampard wametajwa kuwa miongoni wa viungo 15 waliopo katika orodha itakayounda kikosi cha dunia 2012 maarufu kama FIFPro. Eden Hazard, David Silva na Yaya Toure ni miongoni mwa wachezaji wengine ambao wanacheza katika Ligi Kuu nchini uingereza ambao nao wametajwa katika orodha hiyo. Viungo watatu kati ya hao ndio watachaguliwa kuunda kikosi cha dunia majina ambayo yatatangazwa wakati wa sherehe za utoaji tuzo ya mchezaji bora wa dunia maarufu kama Ballon d’Or Januari 7 mwakani. Klabu ya Barcelona imetoa wachezaji viungo wanne kwenye orodha hiyo ambao ni Sergio Busquets, Csec Fabregas, Andres Iniesta na Xavi Hernandez ambao waliisaidia timu ya taifa ya Hispania kutetea taji lao la Ulaya. Mbali na hao wachezaji wengine waliokuwepo katika orodha ya viungo 15 pamoja na nchi na vilabu wanavyotoka ni pamoja na Xabi Alonso-Hispania na Real Madrid, Luka Modric-Croatia na Real Madrid, Mesut Ozil-Ujerumani na Real Madrid. Wengine ni Andrea Pirlo-Italia na Juventus, Franck Ribery-Ufaransa na Bayern Munich. David Silva-Hispania na Manchester City, Bastian Schweinsteiger-Ujerumani na Bayern Munich.

No comments:

Post a Comment