Tuesday, November 27, 2012

BRAZIL WACHOMOA KUMUHITAJI GUARDIOLA.

RAIS wa Shirikisho la Soka la Brazil, Jose Maria Marin amekanusha taarifa kuwa watamteua kocha wa zamani wa Barcelona Pep Guardiola kukiongoza kikosi cha nchi hiyo katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014. Marin amesema kuwa kuna nafasi ndogo sana wa kuchukua kocha mgeni kwani wameshinda mara tano michuano ya Kombe la Dunia wakiwa na kocha mzawa hivyo hawaoni umuhimu wa kuwa na kocha wa kigeni katika kampeni za michuano ya 2014. Chanzo kimoja cha habari kilichokaribu na Guardiola kilidai Jumamosi kuwa Brazil ndio timu pekee ambayo kocha huyo yuko tayari kufundisha baada ya Mano Menezes kutimuliwa baada ya kuinoa timu hiyo kwa miaka miwili na nusu. Wakati akiinoa Brazil, Menezes amekiongoza kikosi cha nchi hiyo kushinda michezo 21 kati ya 40 ukiwemo mchezo wa fainali ya olimpiki ambao walipoteza kwa Mexico na kukosa medali ya dhahabu.

No comments:

Post a Comment