Tuesday, November 27, 2012

SIMEONE AFURAHISHWA NA KIWANGO CHA ATLETICO.

MENEJA wa klabu ya Atletico Madrid, Diego Simeone ameonyesha kufuruhishwa na kiwango cha timu yake katika msimu huu wa Ligi Kuu nchini Hispania maarufu kama La Liga. Atletico wamefanikiwa kushinda michezo yao 13 kati ya 15 waliyocheza katika ligi hiyo na wapo nyuma kwa vinara wanaaongoza ligi hiyo Barcelona kwa alama tatu. Simeone aliwasifia wachezaji wake kwa kiwango walichokionyesha katika mchezo dhidi ya Sevilla Jumapili iliyopita na kufanikiwa kuibuka na ushindi mnono wa mabao 4-0. Hatahivyo kocha huyo alikataa kuzungumzia mchezo wa la Liga dhidi ya Real Madrid ambao utachezwa Jumamosi kwasababu ya mchezo wa Copa del Rey dhidi ya Real Jean ambao wanatarajia kucheza katikati ya wiki hii. Simeone ambaye ana umri wa miaka 42 amesema kuwa haitakuwa jambo la busara kuwazungumzia Real Madrid na kuwadharau Real Jean ambao wanatarajiwa kucheza nao kabla ya Real.

No comments:

Post a Comment