Tuesday, November 27, 2012

WAZO LA KUONGEZA NCHI WENYEJI KATIKA MICHUANO YA EURO 2020 KUJADILIWA BRUSSELS.

KWA mujibu wa Chama cha soka cha Ujerumani-DFB mpango wa kuandaa michuano ya Ulaya mwaka 2020 katika nchi zote za bara hilo tofauti na nchi moja au mbili kama ilivyo hivi sasa linaonekana kuungwa mkono na mashirikisho mengi mengi ya soka barani humo. Kuelekea mkutano wa siku mbili wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA ambao utafanyika jijini Brussels, Katibu Mkuu wa DFB Helmut Sandrock amesema kuwa mara ya kwanza walishangazwa na wazo hilo lililotolewa na rais wa UEFA Michel Platini. Pendekezo hilo ambalo bado halijapitishwa na Kamati ya Utendaji ya UEFA litashuhudia nchi 12 mwenyeji wa michuano hiyo ambayo itajumuisha nchi 24 zitakazoshiriki tofauti na 16 kama ilivyo hivi sasa. Sandrock aliendelea kusema kuwa mara ya kwanza walishangazwa na wazo hilo lakini baadae walikaa chini kama DFB kuangalia upya pendekezo hilo na kuona kama kweli linafaa wazo linaonekana linawezekana. Platini alitoa wazo hilo la kuongeza nchi wenyeji kwenye michuano hiyo ili kupunguza muda mrefu wa maandalizi pamoja na gharama ambazo nchi hupata wakati wa maandalizi ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment