Thursday, November 22, 2012

WATANO KUGOMBEA TUZO YA BBC AFRICAN PLAYER OF THE YEAR.

MAJINA matano ya wachezaji watakaogombea tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika mwaka huu ambayo inatolewa na Shirika la Utangazaji la Uingereza la BBC yametangazwa rasmi. Majina ya wachezaji hao ni pamoja na Yaya Toure ambaye anaingia katika orodha hiyo kwa mara ya pili mfululizo akiungana na nyota mwenzake kutoka Ivory Coast, Didier Drogba, Demba Ba kutoka Senegal, Younes Belhanda kutoka Morocco na nahodha wa Zambia Christopher Katongo. Mshindi wa tuzo hiyo ataamuliwa na mashabiki wa soka barani Afrika Afrika ambao wanatapa nafasi ya kupiga kura mpaka Alhamisi Desemba 13 mwaka huu ya kuchagua mchezaji wanayedhani amefanya vizuri. Wachezaji hao wamechaguliwa kugombea tuzo hiyo kutokana na kufanya vizuri kwa mwaka huu katika vilabu na timu zao za taifa ambapo mshindi anatarajiwa kutangazwa Jumatatu Desemba 17 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment