Thursday, November 22, 2012

DI MATTEO AELEZA MAPENZI ALIYONAYO KWA CHELSEA PAMOJA NA KUTIMULIWA.

ROBERTO Di Matteo amezungumzia mapenzi yake ya dhati aliyonayo kwa klabu ya Chelsea pamoja na kutimuliwa kuinoa timu hiyo baada ya kukabidhiwa miezi nane iliyopita. Kocha huyo alifanikiwa kushinda kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la FA baada ya kushika nafasi kwa muda baada ya aliyekuwa kocha wa timu Adres Villas Boas kutimuliwa ingawa baadae alipewa mkataba wa miaka miwili. Akihojiwa mara baada ya taarifa za kutimuliwa kutolewa Di Matteo amesema kuwa anajivunia mafanikio aliyopata katika kipindi kifupi alichokuwa meneja wa klabu hiyo ambayo amekuwa na mapenzi nayo kwa kipindi kirefu. Di Matteo alijiunga na Chelsea kama mchezaji mwaka 1996 na kufunga mabao 26 katika michezo 175 aliyocheza kabla ya kuamua kutundika daruga kwasababu ya kuwa majeruhi akiwa na umri wa miaka 31. Aliyewahi kuwa meneja wa Liverpool, Rafael Banitez ndio ameteuliwa kuchukua nafasi ya Di Matteo mpaka msimu huu utakapomalizika.

No comments:

Post a Comment