Thursday, November 22, 2012

CHELSEA YAPANGA KUMREJESHA DROGBA STAMFORD BRIDGE.

KLABU ya Chelsea iko katika mazungumzo ambayo kuna uwezekano wa kuona mshambuliaji wake wa zamani Didier Drogba akirejea Stamford Bridge akitokea klabu ya Shanghai Shenhua ya China kwa mkopo. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 34 anataka kujiweka fiti kwa ajili ya maandalizi ya michuano ya Mataifa ya Afrika 2013 katika kipindi hiki ambacho msimu wa ligi nchini china umemalizika. Drogba ameliomba Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kumpa ruhusa ya kuhama kabla ya kipindi cha usajili cha dirisha dogo Januari mwakani ombi ambalo shirikisho hilo limedai inalishughulikia. Chelsea katika kipindi cha karibuni imekuwa ikikabiliwa na tatizo la mshambuliaji kutokana na Fernando Torres kushuka kiwango huku Daniel Sturridge kuwa majeruhi. Drogba ambaye pia amehusishwa na tetesi za kwenda Liverpool, alikaa katika klabu Chelsea kipindi cha miaka nane baada ya kusajiliwa akitokea Olympique Marseille ya Ufaransa mwaka 2004.

No comments:

Post a Comment