Thursday, November 22, 2012

WENGER SASA ATAKA KUONGOZA KUNDI.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amepanga kutumia kikosi chake cha kwanza katika mchezo wa mwisho wa kundi B wa Ligi ya Mabingwa Ulaya pamoja na timu yake kufuzu hatua ya timu 16 bora. Arsenal ilifanikiwa kutinga katika hatua hiyo baada ya kuifunga Montpellier ya Ufaransa mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika jana lakini wanatarajia kusafiri kuifuata Olympiakos Desemba 4 katika mchezo wa mwisho huku wakiwa katika nafasi ya pili mbele ya Schalke 04 ambao wanaongoza kundi hilo. Wenger amesema kuwa amepanga kutumia kikosi chake kamili katika mchezo huyo ili kujaribu kushinda na kumaliza wakiwa vinara wa kundi hilo kitu ambacho kitakuwa muhimu. Kama wakimaliza vinara katika kundi lao watapangiwa timu ambazo zimeshika nafasi ya pili katika makundi mengine na kama wakishindwa kufanya hivyo na kumaliza katika nafasi ya pili watapangiwa kucheza na washindi wa makundi mengine katika hatua inayofuata ya michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment