Wednesday, November 28, 2012

ZICO AJIUZULU KUINOA IRAQ.

ALIYEKUWA kocha wa timu ya taifa ya Iraq, Zico ameamua kujiuzulu wadhfa wake huo baada ya kudai kuwa Shirikisho la Soka la nchi hiyo limeshindwa kufikia makubaliano waliyokubaliana katika mkataba wake. Kujiuzulu kwa Zico ambaye ni nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil kumekuja ikiwa bado Iraq inapigania nafasi ya kushiriki michuano ya Kombe la Dunia 2014 itakayofanyika nchini Brazil. Iraq inashika nafasi ya tatu katika kundi B kwa timu za uapnde wa bara la Asia wakiwa na alama 5 katika michezo mitano waliyocheza wakipishana alama moja na Australia ambao wako katika nafasi ya pili huku Japan akiongoza kundi hilo kwa alama 13. Timu mbili ndio zitafuzu moja kwa moja kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2014 wakati timu itakayoshika nafasi ya tatu itakwenda katika hatua ya mtoano. 

No comments:

Post a Comment