Monday, December 24, 2012

CASILLAS AKATAA KUMKOSOA MOURINHO.

NAHODHA wa klabu ya Real Madrid, Iker Casillas amekataa kukosoa maamuzi ya kocha wake Jose Mourinho baada ya kumuweka benchi katika mchezo wa Jumamosi ambao walifungwa mabao 3-2 na Malaga. Uamuzi wa kumuacha Casillas ulielezewa na kocha huyo Mreno kama la kiufundi lakini ilisababisha Madrid kupoteza alama tatu muhimu katika mchezo huo wa La Liga. Akihojiwa Casillas amekiri kuwa hakuzoea hali hiyo ya kutocheza lakini siku zote kocha ndio anachagua nani acheze na asicheze hivyo akiwa kama mchezaji lazima aheshimu maamuzi yao kocha. Amesema wachezaji wenzake wote wamekuwa wakimfariji kama walivyokuwa wakimfariji Antonio Adan ambaye ni golikipa namba mbili aliyechukua namba ya Casillas katika mchezo dhidi ya Malaga. Suala la Mourinho kumuacha Casillas limechukuliwa tofauti na wadau wengi wa soka mmojawapo akiwa mkurugenzi wa zamani wa michezo wa Madrid Jorge Valdano ambaye anaamini kuwa kocha huyo alikuwa akifikisha ujumbe kwamba yeye ndiye bosi katika klabu hiyo. 

No comments:

Post a Comment