Monday, December 24, 2012

CHELSEA YAVUTA PAUNDI MILIONI 12 KWA STURRIDGE.

KLABU ya Chelsea imekubali kumuuza mshambuliaji wake Daniel Sturridge kwenda Liverpool kwa ada ya paundi milioni 12. Mshambuliaji huyo ambaye alifanyiwa vipimo vya afya Jumapili anategemewa kusaini mkataba wa miaka mitatu na nusu na Liverpool katika muda wa saa 24 zijazo. Mshambuliaji huyo ambaye alikuwa akitaka kupigania namba Chelsea mpaka mkataba wake utakapomalizika mizei 18 ijayo, atakuwa akilipwa na Liver mshahara wa paundi 60,000 kwa wiki. Chelsea itakuwa imepata faida kubwa kwa kumuuza mshambuliaji huyo ambaye walimnunua kwa ada ya paundi milioni 1.5 akitokea klabu ya Manchester City mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment