Monday, December 24, 2012

MDOGO WAKE BALOTELLI AKAMATWA.

KAKA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Italia, Mario Balotelli alikamatwa Jumapili kwa tuhuma za kujeruhi maofisa wawili wa polisi wakati wa vurugu zilizotokea mtaani. Enoch Barwuach ambaye ni mdogo wake Balotelli ambaye anacheza katika klabu ya Manchester City anakabiliwa na mashtaka ya kushambulia na kukataa kukamatwa baada ya kujihusisha na ugomvi katika klabu ya usiku Jumamosi huko Brescia, Italia. Barwuah mwenye umri wa miaka 20 ambaye amezaliwa tumbo moja na Balotelli alilala lupango kabla ya kuhamishwa ambapo anatarajiwa kupelekwa mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili. Mdogo wake Balotelli ameonyesha kufuata nyendo za kaka yake ambaye amekuwa akikumbwa na matukio mbalimbali ya vurugu ndani na nje ya uwanja.

No comments:

Post a Comment