Tuesday, December 4, 2012

MESSI ANASTAHILI BALLON D'OR - NEYMAR.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Santos ya Brazil, Neymar anaamini kuwa Lionel Messi atashinda Ballon d’Or mbele ya mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo kutokana na kiwango bora alichokionyesha msimu huu. Kwa mwaka huu pekee Messi amefunga mabao 84 katika mechi za kimataifa na klabu na Neymar mwenye umri wa miaka 20 anaamini kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Argentina anastahili tuzo hiyo kutokana na kiwango alichokionyesha. Neymar amesema kuwa ingawa anadhani mshindi atakuwa Messi lakini hata Ronaldo naye amekuwa msimu mzuri hivyo kitakuwa kinyang’anyiro cha kuvutia katika tuzo hizo za Ballon d’Or. Nyota huyo pia aliendelea na msimamo wake wa kubakia Santos mpaka mkataba wake utakapoisha mwaka 2014 ndipo atafikiria kama aende Ulaya au aendelee kubakia Brazil kwa kipindi kingine. Amesema anazo ndoto za kwenda kucheza soka Ulaya lakini kwasasa anafurahia kuwepo Santos kwakuwa anakuwa karibu na familia yake pamoja na marafiki.

No comments:

Post a Comment