Tuesday, December 4, 2012

QUIT SMOKING WITH BARCA CAMPAIN.

KLABU ya Barcelona ya Hispania imeungana na Tume ya Ulaya kusaidia mashabiki wa soka kuacha kuvuta sigara. Baadhi ya wachezaji nyota wa klabu hiyo wakiwemo Andres Iniesta, Xavi Hernandez na Carles Puyol wako katika kampeni hiyo wakitaka mashabiki kusema hapama kuvuta sigara na wamejitolea kutoa mwongozo na msaada kwa mashabiki ambao wanataka kuachana na suala la kuvuta sigara. Kampeni hiyo iliyoanzishwa na klabu hiyo ambayo inaitwa Quit Smoking with Barca pia iko katika mitandao ya internet na simu za mkononi ambapo mashabiki wa klabu hiyo watakuwa wakipata maelezo ya jinsi gani ya kuacha kuvuta sigara na kupewa hamasa kutoka kwa wachezaji, kocha Tito Vilanova pamoja na rais wa klabu hiyo Sandro Rosell. Katika kampeni hiyo ya mtandao ambayo inaitwa FCB iCoach mvutaji sigara atahitajika kuingia na kujibu maswali rahisi kabla ya kuanza kupata maelezo mbalimbali ya kukabiliana au kuachana kabisa na tabia hiyo ya kuvuta sigara. Kukiwa na zaidi wavutaji sigara milioni 140 kuzunguka bara la Ulaya, Tume ya Ulaya inaamini kuwa muonekano wa klabu hiyo ambayo ni kubwa duniani utasaidia kwa kiasi kikubwa kupambana na suala hilo. 

No comments:

Post a Comment