Tuesday, December 4, 2012

MESSI KUVUNJA REKODI YA MULLER KATIKA MCHEZO DHIDI YA BENFICA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona Lionel Messi amepata nafasi nyingine ya kufikia rekodi ya mabao 85 ambayo yalifungwa na Gerd Muller katika kipindi cha mwaka mmoja baada ya kocha wa timu hiyo Tito Vilanova kumjumuisha katika kikosi chake kitakachopambana na Benfica katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya. Messi mwenye mabao 84 hivi sasa amebakisha bao moja kufikia rekodi ya miaka 40 ambayo iliwekwa na Muller ambaye ni mshambuliaji wa zamani wa Ujerumani na klabu ya Bayern Munich. Vilanova amesema kuwa ameamua kumtumia Messi na kuwapumzisha nyota wengine kwasababu mchezaji huyo alipumzika katika mchezo wa Kombe la Mfalme wiki iliyopita. Nyota wa klabu hiyo waliopumzishwa ni pamoja na Andres Iniesta, Xavi Hernandez, Javier Mascherano, Pedro, Jordi Alba na Cesc Fabregas ambapo nafasi zitachukuliwa na wachezaji vijana kutoka katika akademi ya klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment