Tuesday, December 4, 2012

MSHINDI WA BALLON D'OR TAYARI AMESHAJULIKANA.

MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Jose Mourinho amedai kuwa mshidi wa tuzo ya Ballon d’Or tayari ameshaamuliwa kwa kuwatuhumu Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kumpigia debe nyota wa Barcelona Lionel Messi. Messi ndio anayepewa nafasi kubwa ya kunyakuwa tuzo hiyo ya mchezaji bora duniani kwa mara ya tatu mfululizo lakini anakabiliwa na upinzani kutoka kwa mchezaji mwenzake kutoka Barcelona Andres Uniesta na mshambuliaji nyota wa Madrid Cristiano Ronaldo. Kauli hiyo ya Mourinho ilikuja wakati akiulizwa kama Ronaldo ana nafasi ya kunyakuwa Ballon d’Or baada ya ushindi wa mabao 4-1 iliyopata Madrid dhidi ya Ajax jana katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya. Akijibu swali hilo Mourinho amesema kuwa wakati FIFA wakiongea na kufanya kampeni hakuna unaloweza kufanya hivyo anadhani tuzo ya Ballon d’Or tayari imeshatolewa. 

No comments:

Post a Comment