Tuesday, December 4, 2012

SIJAHUZUNISHWA NA UAMUZI WA FIFA - DROGBA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Ivory Coast, Didier Drogba amesema kuwa hajakasirishwa na uamuzi wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kumkatalia ombi lake la kuondoka Shanghai Shenhua kwa mkopo kwenda katika klabu yake ya zamani Chelsea kabla ya kipindi cha dirisha la usajili kufunguliwa. Drogba amesema hakutegemea kukubaliwa kwa ombi lake kutoka kwa shirikisho hilo kwasababu ni kitu kisicho cha kawaida na hakukuwa na dhamana kwamba kitakubalika. Nyota huyo ambaye kwasasa anafanya mazoezi katika klabu yake hiyo ya zamani kwa ajili ya kujiwenda na michuano ya Mataifa ya Afrika yakayoanza Januari 19 mwakani amesema kukataliwa huko hakuwezi kumkosesha usingizi kwakuwa alikuwa anajaribu. Katika taarifa yake FIFA imesema kuwa ombi la mchezaji huyo lingewezekana kama mkataba wake ungekuwa umeisha wakati wa dirisha la usajili bado halijafunguliwa lakini Drogba bado ana mkataba na Shenhua mpaka 2015.

No comments:

Post a Comment