Monday, December 10, 2012

SIJAWAHI KUKUTANA NA MTU KAMA MOURINHO - ETO'O.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Cameroon, Samuel Eto’o amesema kuwa hajawahi kukutana na mtu wa aina ya Jose Mourinho katika maisha yake. Wawili hao walifanya kazi pamoja wakati mourinho akiinoa Inter Milan na Eto’o kuweka wazi kuwa walipata wakati mgumu wakati kocha huyo alipoondoka katika klabu hiyo na kwenda kuinoa Real Madrid mwaka 2010. Eto’o anemuelezea Mourinho kama mtu muungwana na kocha mzuri na kuwa mmoja wa watu wachache wa aina yake ambao amewahi kukutana nao ambapo katika mwaka huo walishinda mataji matatu makubwa muhimu. Nyota huyo pia alizungumzia muda aliokuwa chini ya kocha wa zamani wa Barcelona Pep Guardiola na kukiri kuwa alipata wakati mgumu wakati akiondoka katika klabu hiyo lakini alidai kuwa mpaka sasa wana mahusiano mazuri na kocha huyo.

No comments:

Post a Comment