Monday, December 24, 2012

VAN ANA BAHATI KUWA HAI - FERGUSON.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, Sir Alex Ferguson amedai kuwa beki wa Swansea City Ashley Williams angewewa kumuua Robin van Persie wakati wa mchezo baina ya timu hizo uliochezwa katika Uwanja wa Liberty jana. Beki huyo wa kimataifa wa Wales alipiga mpira uliomgonga kichwani Van Persie katika kipindi cha pili na kupelekea mshambuliaji huyo kunyanyuka kwa hasira na kumvaa Williams na wote kupelekea kupewa kadi nyekundu. Ferguson amesema kuwa tukio hilo ni bay asana kwani lingeweza kusababisha madhara makubwa kama kifo hivyo aliomba Chama cha Soka cha Uingereza-FA kuchunguza na kutoa adhabu. Williams akihojiwa mara baada ya mchezo huo alidai kuwa lilikuwa tukio la bahati mbaya hakudhamiria kumbutua na mpira kichwani Van Persie na kusababisha nyota huyo kushikwa na jazba. Mchezo huo ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 hiyo ikiwa ni sare ya kwanza United katika michezo 21 waliyocheza ambapo bado wamebakia kileleni mwa Ligi Kuu nchini humo wakiongoza kwa alama 43.

No comments:

Post a Comment