Wednesday, January 23, 2013

AFCON 2013: MAHUDHURIO BADO SIO YAKURIDHISHA.

PAMOJA na mahudhurio mabovu, hali ya hewa imekuwa nzuri karibu kila mechi katika michezo nane ya ufunguzi wa michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon inayoendelea nchini Afrika Kusini. Mahudhurio madogo sio kitu cha kushangaza katika mechi za ufunguzi za mashindano ya Afrika lakini kujua haswa idadi ya mashabiki waliohudhuria huwa ni kitu kigumu kwakuwa Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF na kamati ya maandalizi huwa mara chache ndio huzungumzia idadi kamili ya waliohudhuria. Siti tupu viwanjani zimekuwa hazileti muonekano mzuri wa mashindano hayo katika picha za luninga zinazoonyeshwa duniani kote, ingawa hata hivyo mashabiki hao wachache, na hali nzuri ya hewa ni vitu ambavyo vimekuwa vikileta msisimko katika michuano hiyo. Kelele za vuvuzela, filimbi za plastiki zilizojizolea umaarufu mkubwa katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010 mpaka watu wengine hususani wa mataifa ya Ulaya kuzipiga marufuku katika viwanja vyao ndio zimekuwa zikiweka uhai uwanjani katika michuano ya mwaka huu.

No comments:

Post a Comment