Wednesday, January 23, 2013

AUSTRALIA OPEN: FEDERER KUKWAANA NA MURRAY NUSU FAINALI.

MCHEZA anayeshika namba mbili katika orodha za ubora, Roger Federer wa Switzerland amefanikiwa kumfunga Jo-Wilfried Tsonga katika robo fainali ya michuano ya wazi ya Australia inayoendelea jijini Melbourne. Federer alifanikiwa kumfunga kwa tabu Tsonga kwa 7-6 4-6 7-6 3-6 6-3 na sasa atakutana na Andy Murray wa Uingereza katika hatua ya nusu fainali baada ya muingereza huyo kumuondosha Jeremy Chardy wa Ufaransa. Kwa upande wanawake bingwa mtetezi wa michuano hiyo Victoria Azarenka alimfunga Svetlana Kuznetsova na kujihakikishia nafasi ya kucheza nusu fainali ya michuano hiyo. Mwanadada huyo anayeshika namba katika orodha za ubora duniani sasa atakutana na chipukizi mwenye miaka 19 Sloane Stephens wa Marekani ambaye alimuondosha Serena Williams katika robo fainali.

No comments:

Post a Comment