Wednesday, January 23, 2013

BUFFON KUSTAAFU AKIWA JUVENTUS.

VYOMBO vya habari nchini Italia vimeripoti kuwa golikipa wa kimataifa wa Italia Gianluigi Buffon anatarajia kusaini mkataba mpya na mabingwa wa Serie A klabu ya Juventus utakaodumu mpaka 2015. Buffon ambaye amefikisha miaka 35 Jumatatu anategemea kusaini mkataba utakaokuwa na thamani ya euro milioni nne kwa kila msimu ikiwa ni punguzo la moja ya tatu ya mkataba wake unaoishia. Meneja wa Juventus Antonio Conte alikaririwa akisema kuwa Buffon ni mojawapo ya makipa bora kabisa duniani na amefurahi kwamba atabaki nao. Buffon ambaye alikuwemo katika kikosi cha timu ya taifa ya Italia kilichonyakuwa Kombe la Dunia mwaka 2006 alitua Juventus mwaka 2001 na kufanikiwa kushinda mataji matatu ya Serie A na matatu ya Kombe la Italia.

No comments:

Post a Comment