Thursday, January 24, 2013

BAGGIO AJIUZULU UKURUGENZI WA KICHEZO ITALIA.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Italia, Roberto Baggio amejiuzulu wadhifa wake kama mkurugenzi wa ufundi wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo akidai kuzuiwa kufanya kazi yake aliyotaka. Nyota huyo wa zamani ambaye alikuwepo katika kikosi cha Italia kilchomaliza katika nafasi ya pili kwenye michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1990 na 1994 aliteuliwa kushika wadhifa huo baada ya kikosi cha timu ya taifa wakiwa kama mabingwa watetezi kushindwa kupenya katika hatua ya makundi kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2010. Baggio amesema kuwa aliwasilisha mawazo yake yaliyokuwa na kurasa 900 kwa shirikisho hilo mojawapo likiwa kujaribu kuinua vipaji vya vijana lakini hakujibiwa chochote ndio maana akaamua kujiuzulu. Italia ilimaliza katika nafasi ya pili katika michuano ya Ulaya mwaka jana baada ya kufungwa na Hispania chini ya kocha Cesare Prandelli.

No comments:

Post a Comment