Thursday, January 24, 2013

Hazard RED CARD Kicks BALLBOY in the RIBS | Swansea 0-0 Chelsea


MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Ubelgiji na klabu ya Chelsea, Eden Hazard ameomba radhi kwa kumpiga muokota mipira ambaye alikuwa akimzuia kuchukua mpira katika nusu fainali ya Kombe la Ligi dhidi ya Swansea City jana. Hazard ambaye alitolewa nje, alikutana na kijana huyo aitwaye Charlie Morgan ambaye ni mtoto wa mkurugenzi wa Swansea Martin Morgan katika chumba cha kubadilishia nguo na kumuomba radhi kwa kitendo alichomfanyia. Swansea ambao walishinda mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza uliochezwa katika Uwanja wa Stamford Bridge walifanikiwa kuwazuia Chelsea na kupata sare ya bila ya kufungana katika Uwanja wa Liberty na kujikatia tiketi ya kucheza fainali na Bradford City. Katika maelezo yake Hazard amesema hakudhamiria kumpiga mateke kijana huyo kama inavyoonekana kwani alichodhamiria yeye ni kupiga mpira lakini kwakuwa kijana huyo alikuwa ameulalia ndio maana akaonekana kama anampiga. Nyota huyo aliendelea kusema alizungumza na tayari ameshamuomba msamaha kijana huyo alipokuja katika chumba cha kubalishia nguo mara baada ya kumalizika mchezo huo hivyo suala hilo limekwisha.

No comments:

Post a Comment