Thursday, January 24, 2013

AUSTRALIA OPEN: AZARENKA, LI NA KUKWAANA FAINALI.

BINGWA mtetezi wa michuano ya wazi ya Australia, Victoria Azarenka amefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano hiyo baada ya kumfunga mbabe wa Serena Williams, Sloane Stephens katika mchezo wa nusu fainali uliochezwa jijini Melbourne. Katika mchezo huo Azarenka aliondoka uwanjani kwa karibu dakika 10 ili kupata matibabu lakini baadae alirejea tena na kufanikiwa kumfunga Stephanes kwa 6-1 6-4. Mwanadada huyo raia wa Belarus mwenye umri wa miaka 25 anayeshika namba moja katika orodha za ubora duniani sasa atakutana na Li Na katika hatua ya fainali baada ya mwanadada huyo kutoka China kumuondosha Maria Sharapova wa Urusi. Li Na mwenye umri wa miaka 30 aliyekuwa katika kiwango bora alifanikiwa kumfunga Sharapova anayeshika namba mbili katika orodha za ubora kwa 6-2 6-2 akitumia muda wa dakika 93.

No comments:

Post a Comment