Thursday, January 24, 2013

AUSTRALIA OPEN: DJOKOVIC ATINGA FAINALI.

BINGWA mtetezi wa michuano ya wazi ya Australia, Novak Djokovic amefanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo kwa kumgaragaza David Ferrer na kufanikiwa kujiweka katika nafasi nzuri ya kunyakuwa taji hilo kwa mara ya tatu mfululizo. Katika mchezo huo Djokovic raia wa Serbia alimfunga Ferrer anayetoka Hispania kwa 6-2 6-2 6-1 akitumia muda wa saa moja na dakika 29 ambapo sasa anasubiri mshindi katika mchezo mwingine wa nusu fainali kati ya Roger Federer na Andy Murray. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Djokovic amesema ulikuwa mchezo rahisi kuliko alivyotegemea kwani alianza vizuri kwa kujiamini toka mwanzo na kucheza katika kiwango bora kabisa. Kama akifanikiwa kuchukua taji hilo katika fainali itakayochezwa Jumapili atakuwa mchezaji wa kwanza kwa upande wa wanaume toka kuanzishwa kwa mashindan hayo ya wazi mwaka 1968.

No comments:

Post a Comment