Thursday, January 24, 2013

REAL MADRID YAONGOZA KWA KUINGIZA FEDHA NYINGI.

KLABU ya Real Madrid imeendelea kuongoza katika orodha za vilabu vinavyoingiza fedha nyingi zaidi duniani baada ya kuwa klabu ya kwanza ya michezo kuingiza kiasi cha euro milioni 500 kwa msimu mmoja. Mapato hayo ambayo wameyapata katika msimu wa mwaka 2011-2012 yanawafanya kuongoza katika orodha hiyo kwa misimu nane mfululizo wakifuatiwa na mahasimu wao Barcelona ambao wanashika nafasi ya pili kwa kuingiza kiasi cha euro milioni 483 msimu uliopita. Nafasi ya tatu katika orodha hiyo inakwenda kwa Manchester United ambao msimu uliopita waliingiza kiasi cha euro milioni 395.9 wakifuatiwa na Bayern Munich katika nafasi ya nne euro milioni 368.4 huku ya tano ikishikiliwa na Chelsea wanaoingiza euro milioni 322.6. Arsenal wameporomoka mpaka nafasi ya sita kutoa nafasi ya nne waliokuwepo msimu wa mwaka juzi kwa kuingiza kiasi cha euro milioni 290.3, Manchester City wamekwea mpaka nafasi ya saba kwa kuingiza euro milioni 285.6 wakifuatiwa na AC Milan katika nafasi ya nane euro milioni 256.9. Timu nyingine ni Liverpool inayoshika nafasi ya tisa kwa kuingiza kitita cha euro 233.2 na kumi bora inafungwa na bibi kizee wa Turin klabu ya Juventus walioingiza kiasi cha euro 195.4. 

TOP 20: (All figures in millions of euros)
1. Real Madrid (Spain) 512.6 
2. Barcelona (Spain) 483
3. Manchester United (England) 395.9
4. Bayern Munich (Germany) 368.4
5. Chelsea (England) 322.6
6. Arsenal (England) 290.3
7. Manchester City (England) 285.6
8. AC Milan (Italy) 256.9
9. Liverpool (England) 233.2
10. Juventus (Italy) 195.4
11. Borussia Dortmund (Germany) 189.1
12. Inter Milan (Italy) 185.9
13. Tottenham Hotspur (England) 178.2
14. Schalke 04 (Germany) 174.5
15. Napoli (Italy) 148.4
16. Olympique Marseille (France) 135.7
17. Olympique Lyon (France) 131.9
18. Hamburg SV (Germany) 121.1
19. AS Roma (Italy) 115.9
20. Newcastle United (England) 115.3

No comments:

Post a Comment