Friday, January 25, 2013

BARCELONA KUWAKARIBISHA WACHOVU OSASUNA.

VINARA wa Ligi Kuu nchini Hispania, maarufu kama La Liga Barcelona inatarajia kuikaribisha Osasuna Jumapili ili kujaribi kurejesha makali yao baada ya kupata kipigo cha kwanza 3-2 dhidi ya Real Sociedad katika ligi hiyo Jumamosi iliyopita. Barcelona ambao waliweka rekodi katika nusu ya kwanza ya msimu kwa kupoteza alama mbili pekee wanaongoza La Liga wakiwa juu ya Atletico Madrid wanaoshika nafasi ya pili kwa alama nane huku mahasimu wao Real Madrid wakiwa katika nafasi ya tatu kwa tofauti ya alama 15. Hata hivyo mwishoni mwa iliyopita Barcelona alijikuta wakipoteza mchezo baada ya kuongoza kwa mabao mawili mapema katika kipindi cha kwanza na hiyo imekuwa kama tahadhari kwao wakati kukiwa kumebakiwa mechi 18 kabla ya ligi hiyo kumalizika. Pamoja na kipigo hicho, Barcelona imeonyesha katikati ya wiki hii kwamba tayari wameshasahau wakati walipoigaragaza Malaga mabao 4-2 katika robo fainali ya pili ya Kombe la Mfalme na kutinga hatua ya nusu fainali ambapo sasa watakutana na Madrid. Katika mchezo wa Jumapili Barcelona itamkosa beki wake tegemeo Gerard Pique ambaye alipewa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Sociedad.

No comments:

Post a Comment