Friday, January 25, 2013

UEFA YATAKA UKOMO WA URAIS FIFA UWE MIAKA 12.

Maofisa wa soka barani Ulaya wametaka kikomo cha urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kuwa miaka 12 ikiwa ni miaka minne zaidi ya mshauri wa mambo ya rushwa wa shirikisho hilo alivyoshauri. Katika taarifa yake UEFA wamesema kuwa wajumbe wake kutoka mataifa 53 wamependekeza kuwa FIFA wafuate utaratibu wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki kwa rais wake kukaa madarakani kwa kipindi cha miaka 12. Rais wa sasa wa FIFA Sepp Blatter atamalizia miaka yake 17 akiwa katika nafasi hiyo wakati kipindi chake kitakapomalizika mwaka 2015. Rais wa UEFA Michel Platini ambaye amesema hata gombea tena nafasi hiyo kipindi chake kitakapomalizika ndio anayepewa nafasi kubwa ya kumrithi Blatter baada ya kuondoka. Lakini bado mapendekezo ya UEFA bado yanatofautiana na mshauri wa FIFA Mark Pieth ambaye alipendekeza kikomo cha urais wa shirikisho hilo kuwa miaka nane ili kusadia kupunguza mambo ya rushwa na ufisadi.

No comments:

Post a Comment