Friday, January 25, 2013

FENERBAHCE KUCHEZA EUROPA LEAGUE UWANJA MTUPU.

KLABU ya Fenerbahce ya Uturuki italazimika kucheza mchezo wao wa nyumbani wa michuano ya Europa League huku milango ikiwa imefungwa baada ya mashabiki wake kurusha mafataki na vitu ningine uwanjani wakati wa mchezo dhidi ya Borussia Moenchengladbach Desemba mwaka jana. Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA pia limeitoza faini Fenerbahce ya euro 40,000 kwa vurugu hizo zilizotokea katika Uwanja wa Sukru Saracoglu nchini Ujerumani Desemba 6 ambapo Borussia ilishinda kwa mabao 3-0. Katika taarifa yake UEFA imesema kuwa imeamua kutoa adhabu kwa klabu hiyo baada ya kufanya tukio kama hilo tena katika mchezo wa mtoano wa michuano ya Klabu Bingwa arani Ulaya dhidi ya Spartak Moscow Agosti mwaka jana. Fenerbahce itaitumikia adhabu hiyo katika mzunguko wa timu 32 kwenye mchezo wa pili dhidi ya klabu ya BATE Borisov ya Belarus Februari mwaka huu.

No comments:

Post a Comment