Friday, January 25, 2013

PIQUE AMZAWADIA BAO MWANAE MILAN.

BEKI wa kimataifa wa Hispania na klabu ya Barcelona Gerard Pique amemzawadia bao aliloshinda katika mchezo wa jana dhidi ya Malaga mtoto wake wa kiume aliyezaliwa Januari 22. Katika mchezo huo wa jana wa Kombe la Mfalme ambao Barcelona ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 Pique alifunga bao la pili mwanzoni mwa kipindi cha na kushangiliwa huku ameweka kidole chake mdomoni. Mtoto huyo aitwaye Milan Pique Mebarak akichukua jina la babu yake kwa upande wa baba yake na pia kwa upande wa mama yake mwanamuzi nyota wa muziki wa pop Shakira Mebarak. Katika taarifa nyingine beki wa Barcelona Eric Abidal amerejea tena hospitali kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu baada ya kufanyiwa upasuaji wa kupandikiza ini April mwaka jana. Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo imedai kuwa Abidal atakaa hospitalini kwa kipindi cha siku tatu mpaka nne ili kuangalia kwa makini maendeleo ya uapndikizaji wa ini aliofanyiwa.

No comments:

Post a Comment