Friday, January 25, 2013

NI DJOKOVIC NA MURRAY FAINALI AUSTRALIA OPEN.

MCHEZAJI tenisi nyota kutoka Uingereza, Andy Murray amefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya wazi ya Australia baada ya kumfunga Roger Federer wa Switzerland katika mchezo nusu fainali uliofanyika katika Uwanja wa Rod Laver Arena jijini Melbourne. Murray anayeshika namba tatu katika orodha za ubora duniani kwa upande wa wanaume alifanikiwa kutinga hatua hiyo baada ya kumfunga Federer anayeshika namba mbili kwa ubora kwa 6-4 6-7 6-3 6-7 6-2. Sasa Murray atakwaana na Novak Djokovic anayeshika namba moja katika orodha hizo katika mchezo wa fainali unaotarajiwa kuchezwa Jumapili. Kwa upande wanawake wanadada nyota kutoka Italia Sara Errani na Roberta Vinci wa Italia wamefanikiwa kushinda taji la michuano hiyo la wawili wawili baada ya kuwafunga Ashleigh Barty na Casey Dellacqua kwa 6-2 3-6 6-2. Errani na Vinci walizima ndoto za Barty na Dellacqua ambao ni raia wa Australia kunyakuwa taji hilo kwa mara ya kwanza kwenye ardhi ya nyumbani kwao. 

No comments:

Post a Comment